Home Makala Ongala Atimuliwa Kmc

Ongala Atimuliwa Kmc

by Dennis Msotwa
0 comments

Uongozi wa Timu ya Kmc Fc umemfuta kazi kocha Kali Ongala kutokana na baadhi ya changamoto zake ndani ya timu hiyo yenye makao yake makuu katika manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Tayari Kali Ongala amefutwa kazi hiyo jumamosi ya mei 03 2025 na hayupo na timu kuanzia muda huo japo barua rasmi ya kufutwa Kazi ameipata Mei 04 2025 siku jumapili.

Licha ya kumtimua Kali ameifanya Kmc kuwa na matokeo mazuri katika ligi kuu ya soka ya Nbc msimu huu tangu ajiunge nayo miezi michache iliyopita.

banner

Katika msimamo wa ligi kuu nchini mpaka sasa Kmc ina alama 30 katika michezo 26 ya ligi ikiwa katika nafasi ya 11.

Kmc inakabiliwa na michezo minne ili kufunga pazia la ligi kuu ya Nbc msimu huu ambapo katika michezo hiyo minne umo mmoja dhidi ya Simba Sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited