Home Soka Bodi Ya ligi Yamshukia Zahera

Bodi Ya ligi Yamshukia Zahera

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amepigwa faini ya shilingi laki tano baada ya kuvaa mavazi yasiyo nadhifu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu shooting ambapo timu hiyo ilipoteza kwa bao moja.

Adhabu hiyo imetolewa kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji ligi kuu namba 14(2m) inayohusu taratibu za mchezo.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya kamati ya bodi ya ligi kuu ya uendeshaji na usimamizi wa ligi kukaa kikao septemba 2 ili kupitia matukio mbalimbali ya ligi kuu iliyoanza agosti 24.

banner

Pia klabu ya Yanga nayo imepewa onyo kwa kushindwa kusimamia kocha huyo kuhakikisha anavaa mavazi nadhifu akiwa kama kiongozi wa benchi la ufundi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited