Home Soka Mbappe Kupaa Leo

Mbappe Kupaa Leo

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya vijana (Serengeti boys) Kelvin John 17’ leo atapanda ndege kwenda nchini Ubeligiji kusaini mkataba wa kuichezea rasmi timu ya Krc Genk inayoshiriki ligi kuu nchini humo(Jupiler pro).

Kinda huyo ambaye alikuwemo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya wakubwa(Taifa stars) kilichokwenda nchini Misri kwenye michuano ya mataifa ya Afrika(Afcon 2019) atajiunga na timu hiyo kama mwanafunzi ambaye anasoma nchini humo huku akiwa anaichezea akademi ya timu hiyo.

Hata hivyo kinda huyo ataanza kazi rasmi mwezi Januari wakati wa usajili wa dirisha dogo barani ulaya na tayari ameshaagwa na wachezaji wenzake wa timu ya taifa ya vijana.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited