Home Soka Messi Awabwaga Ronaldo,Van Dijk

Messi Awabwaga Ronaldo,Van Dijk

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Lionel Messi ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa upande wa wanaume akiwabwaga Cristiano Ronaldo na beki wa Liverpool Virgil Van Dijk katika tuzo zilizotolewa usiku huu jijini Milan.

Awali ilidhaniwa beki Van Dijk atachukua tuzo hiyo baada ya kuwa ametwaa ile ya mchezaji bora barani ulaya baada ya kuisadia liverpool kuchukua taji la klabu bingwa barani ulaya.

Hiyo ni mara ya sita kwa staa huyo wa Barcelona akimbwaga hasimu wake Ronaldo aliyechukua tuzo hiyo mara tano akimrithi Luka Modric aliyeshinda tuzo hiyo mwaka jana.

banner

Pia kocha Jurgen Klopp alichukua tuzo ya kocha bora huku kipa Alison Becker pia wa Liverpool alichukua tuzo ya kipa bora.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited