Home Soka Simba Kumenoga,Mo Atema Cheche

Simba Kumenoga,Mo Atema Cheche

by Sports Leo
0 comments

Tajiri wa klabu ya Simba Mohamed Dewji ametoa zawadi za pikipiki,simu za mkononi na rice koka kwa kila mchezaji wa timu hiyo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa kwa timu hiyo endapo itachukua ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara.

Mo aliahidi zawadi ya pikipiki kwa kila mchezaji endapo watatwaa taji hilo lakini ameongeza simu za mkononi na kifaa cha kupikia wali kwa umeme(rice cooker) baada ya timu hiyo kufuzu robo fainali ya michuano ya klabu bingwa afrika kwa msimu ulioisha.

banner

Zawadi hizo zimetolewa na mwakilishi wa makampuni ya mfanyabiashara huyo Fateema Dewji ambapo Simba iliwakilishwa na mtendaji mkuu Senzo Masingiza na kocha Patrick Aussems pamoja na nahodha John Boko huku baadhi ya wachezaji wakihudhuria tukio hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited