Home Soka Nidhamu Kuwaondoa Mkude,Chama

Nidhamu Kuwaondoa Mkude,Chama

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeanza kutafuta mbadala wa wachezaji Cletous Chama na Jonas Mkude kufuatia wachezaji hao kuonyesha nidhamu mbovu katika kikosi hicho.

Katika kuonyesha kuwa wako siriazi na suala la nidhamu tayari mabosi wa timu hiyo wameanza kumfukuzia kiungo mkenya anayecheza kunako klabu ya Zesco United ya Zambia Antony Teddy maarufu kama “Akumu”.

Kiungo huyo mwenye uwezo wa kukaba na kushambulia anamaliza mkataba wake mwezi desemba na tayari mabosi hao wameshaanza mawasiliano na wakala wa mchezaji huyo ambaye huwaletea mastaa klabuni hapo ili kusajili kiungo wakati wa dirisha dogo litakalofunguliwa hivi karibuni na kufungwa desemba.

banner

Mtendaji mkuu wa Simba amesikika akidhibitisha kufanya usajili wa kiungo huyo japo lengo kuu la klabu ni kusajili mshambuliaji atakayesaidiana na Kagere baada ya John Boko kupata majeraha na Wilker  kushindwa kuonesha kiwango.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited