Home Soka Prisons Wamkomalia Mnyama Taifa

Prisons Wamkomalia Mnyama Taifa

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya Prisons imefanikiwa kulazimisha suluhu na Simba sc katika mchezo uliomalizika jioni hii katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam.

Mchezo ulioanza kwa kasi ukitawaliwa na krosi nyingi kuelekea langoni mwa Prisons ulimalizika kwa matokeo hayo baada ya mabeki wa timu hiyo kufanikiwa kuwadhibiti Meddie Kagere na Miraji Athuman huku Cletous Chama na Shiboub wakikosa ubunifu wa kupenyeza mpira langoni mwa wajelajela hao.

Kwa matokeo hayo bado Simba wanaendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 22 huku prisons akipanda mpaka nafasi ya pili akiwa na pointi 19 baada ya kucheza michezo 11.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited