Home Soka K’njaro Queens Yapoteza

K’njaro Queens Yapoteza

by Sports Leo
0 comments

Timu ya taifa ya wanawake nchini(Kilimanjaro queens) imeshindwa kutetea ubingwa wa kombe la Chalenji baada ya jana kufungwa mchezo wa fainali kwa mabao 2-0 na Kenya katika uwanja wa chamazi jijini Dar es salaam.

Jentrix Shikangwa aliyeingia kipindi cha pili ndiye aliyeleta kilio kwa Tanzania baada ya kufunga mabao mawili dakika ya 70 kwa penati baada ya beki wa kilimanjaro queens kuunawa huku akifunga bao la pili dakika ya 87 kwa shuti kali akipokea pasi ya Mwanalima Jereko.

Licha ya kutwaa kombe pia Kenya imetoa golikipa bora,mshambuliaji bora huku Tanzania ikitoa mchezaji bora na timu yenye nidhamu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited