Home Soka Unai Out Arsenal

Unai Out Arsenal

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Arsenal ya nchini England, imemtimua kazi kocha wake Unai Emery kufuatia mwenendo usioridhisha wa timu hiyo kwenye mashindano mbalimbali ikiwemo Ligi Kuu ya England pamoja na Europa League.

Unai anatemwa baada ya kuitumikia klabu hiyo takriban miezi 18 akiwa ameiongoza katika mechi 78, akishinda michezo 43, sare michezo 16 na kupoteza michezo 19.

Kwenye Ligi Kuu ya England ushindi wake ni asilimia 49 huku akiwa na rekodi mbaya zaidi klabuni hapo tangu mwaka 1992 ya kutoshinda mchezo wowote katika mechi saba mfululizo.

banner

Unai raia wa Hispania mwenye umri wa miaka 48, anatimuliwa ikiwa zimepita siku 54 tangu Arsenal ipate ushindi wake wa mwisho na asubuhi ya leo amehudhuria mazoezi ya timu kama kawaida bila kujua litakalomkuta.

Huyu ni kocha wa tatu kutimuliwa kwenye Ligi Kuu ya England msimu huu baada ya Javi Garcia wa Watford na Mauricio Pochettino wa

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited