Home Makala Rwanda Waingia Psg

Rwanda Waingia Psg

by Sports Leo
0 comments

Nchi ya Rwanda imesaini mkataba na timu ya Psg ya nchini Ufaransa ili kupromoti utalii wa nchi hiyo kimataifa huku ikishirikisha mastaa wa timu hiyo kupitia kampeni ya tembelea Rwanda (Visit Rwanda).

Kampeni hiyo mara ya kwanza ilianza kusainiwa kati ya nchi hiyo na Arsenal ambapo inasemekana Rwanda ililipa klabu hiyo dola milioni 44  kwa mkataba wa miaka mitatu huku katika mwaka wa kwanza tu nchi hiyo imeingiza dola za kimarekani milioni 88.

Psg itapromote utalii na bidhaa za nchi hiyo huku bango la “Visit Rwanda”litatokea katika jezi za timu ya wanawake wa klabu hiyo na  kwenye mabango uwanjani.

banner

Japo thamani halisi ya mkataba huyo haijajulikana lakini taarifa zinadai mkataba huo una thamani ya kati ya yuro milioni 6-8.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited