Home Makala Wayne Rooney Amaliza Kifungo

Wayne Rooney Amaliza Kifungo

by Sports Leo
0 comments

Kocha mchezaji wa Derby County inayoshiriki ligi daraja la kwanza England (championship) Wayne Rooney alionekana juzi akiendesha gari kwa mara ya kwanza baaada ya kufungiwa na mahakama kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa mwaka 2017.

Tajiri huyo mwenye magari ya kifahari ya kila aina kama LandRover Overfinch lenye thamani ya pauni 219,00 sawa na sh milioni 656 hakuwa na uwezo wa kuendesha gari kwa miaka miwili licha ya kujaza ndinga kibao nyumbani kwake.

Rooney ametoka Marekani ambako alikuwa anacheza DC United na kutua Derby kutokana na mkewe kutaka kuokoa ndoa yao baada ya mwanassoka huyo kupigwa picha akitoka hotelini Vancouver akiwa na mrembo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited