Home Soka Msuva Hashikiki Morroco

Msuva Hashikiki Morroco

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania anayeitumikia Klabu ya Difaa El Jadidi inayoshiriki Ligi Kuu ya Nchini Morocco (Batola Pro) Simon Msuva  ameendelea Kung’ara baada ya Hapo  Kufunga bao Pekee Lililoipa Ushindi Difaa dhidi ya Vinara wa Ligi Hiyo Wydad Casablanca wakiwa Nyumbani katika mchezo wa ligi kuu nchini humo.

Baada ya Ushindi walioupata Difaa wa Bao 1-0 Wanafikisha Alama 16 na kukamata nafasi ya 7 katika Msimamo wa Ligi Hiyo katika michezo 15 waliyoicheza Huku Vinara wa Ligi Hiyo Wydad Casablanca wanaalama 27 katika michezo 16 Walioicheza .

Baada ya kupachika bao la Ushindi katika Mchezo wa Jana Msuva anashika nafasi ya 3 katika orodha ya wafungaji akiwa na mabao 13 Huku kinara wa Orodha Hiyo Mouhcine lajor kutoka Raja Casablanca anamabao 19 akifuatiwa na Kodjo Laba kutoka RSB Berkane mwenye mabao 19

banner

Ikumbukwe Hili Ni bao la tatu Msuva anaifunga Wydad Casablanca katika michuano mbalimbali nchini humo.

Credit:Yanga Sports Club

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited