Home Makala Mabilioni Ya GSM Yamfanya Mo Kuongea

Mabilioni Ya GSM Yamfanya Mo Kuongea

by Sports Leo
0 comments

Bilionea wa Simba Sc, Mohammed Dewji ‘Mo’ ameanza kutoa maneno  kwa matajiri wa Yanga na kampuni ya GSM iliyomtengea mamilioni kiungo wake Hassan Dilunga ili kuhakikisha anatua Jangwani.

GSM hivi karibuni wapo kwenye mpango wa kumpeleka kiungo huyo Jangwani kwa dau la sh mil 80 kwani ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huu akiwepo na Deo Kanda ambaye naye yupo kwenye mipango ya usajili Yanga.

Kutoka ndani ya kamati ya utendaji wa Simba Sc ,mwekezaji wa klabu hiyo ambaye ni Mo ,amesema hatakubali kumuachia mchezaji yeyote muhimu na tayari ameshaanza mazungumzo na wachezaji hao huku akiwaahidi kuwapatia dau zito kila mmoja wanalotaka ili wasitue yanga.

banner

Mo aliongeza kuwa amepanga kuwabakisha wachezaji wote ambao mkataba wao unakaribia kumeguka kwani wachezaji hao wote wapo kwenye mapendekezo ya ripoti ya kocha Mbelgiji ,Sven Vandenbroeck aliyoikabidhi  kwenye kamati ya usajili wa timu hiyo.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited