Home Makala Jarida La Yanga Kutangazwa Rasmi

Jarida La Yanga Kutangazwa Rasmi

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klabu ya Yanga chini ya Mwenyekiti Dk.Mshindo Msolla,umeandaa jarida maalumu ambalo litakuwa linahusu mambo mbalimbali ya klabu .

Jarida hilo lilizinduliwa Aprili 30 lenye kurasa 48 linalouzwa kwa bei ya shilingi 5000 nchini kote kupitia matawi mbalimbali ya Yanga Sc.

Msolla amesema kuwa jarida hilo limetengenezwa kwa ajili ya mashabiki wa timu hiyo ili kusoma na kufahamu mambo mbalimbali yanayoihusu timu hiyo pia limeambatana na neema kwa mashabiki ambao watanunua jezi za timu hiyo katika maduka ya GSM, watalipata jarida hilo bure.
“Jarida letu hili tumeliandaa kwa ajili ya kuwaelimisha mashabiki wetu mambo mbalimbali yaliyotokea zamani na sasa ambapo jarida hili litapatikana kwa Sh 5000 tu ila kwa wale ambao watanunua jezi za Yanga katika maduka ya GSM watalipata jarida hili bure kabisa” alisema Msolla

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited