Home Makala David Silva Apiga Hesabu Kurejea Valencia

David Silva Apiga Hesabu Kurejea Valencia

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa kikosi cha Manchester City ambao ni mabingwa watetezi wa kombe la ligi kuu England,David Silva amesema kuwa hatakuepo ndani ya timu hiyo msimu ujao wa 2020/21 kwani anaweza kurejea ndani ya timu yake ya zamani ya Valencia huko Hispania.

Kiungo huyo mwenye miaka 34 amesema kuwa hana mpango wa kuendelea kubaki ndani ya kikosi hicho cha Man City msimu ujao pale mkataba wake utamalizika ingawa inaelezwa kuwa City ilitumia nguvu kubwa kumbebeleza nyota huyo abaki ndani ya klabu hiyo ila aligoma kufanya hivyo kwa kuamini kuwa muda wake wa kufanya hivyo umefika.

Manchester City ipo nafasi ya 2 katika msimamo wa ligi kuu England ikiwa na pointi 57 huku Liverpool ikishika nafasi ya kwanza na pointi 82 kibindoni.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited