Home Soka Banka Arejeshwa Yanga

Banka Arejeshwa Yanga

by Sports Leo
0 comments

Joto la pambano la watani wa jadi limezidi kuchukua sura mpya kufuatia kuambatana na matukio lukuki kabla ya pambano hilo litakalofanyika julai 12.

Katika kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo huo wa nusu fainali kombe la shirikisho klabu ya Yanga sc imemrudisha kundini kiungo Mohamed Issa”Mo banka” ambaye alikua amegoma kujiunga na timu hiyo kushnikiza kulipwa stahiki zake za usajili.

Kiungo huyo ambaye alikua na mchango mkubwa katika pambano walilotoka sare raundi ya kwanza baada ya kusababisha goli la pili baada ya kumghasi Mohamed Hussein ambaye alijifunga.

banner

Banka ameitwa kuongeza nguvu kufuatia baadhi ya viungo wa klabu hiyo kuwa majeruhi kama vile Balama Mapinduzi,Haruna Niyonzima na Papy Tshitshimbi hivyo kuilazimu klabu hiyo kumalizana na kiungo huyo haraka na tayari ameshajiunga na timu hiyo kambini mkoani Kagera kujiandaa na mechi dhidi ya Kagera Sugar.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited