Klabu ya Southampton imeharibu ndoto ya mashabiki wengi wa Manchester United ya kumaliza katika nafasi ya nne baada ya kusawazisha bao dakika za lala salama na kufanya matokeo ya mechi hiyo kuwa sare ya 2-2.
Southampton walikua wa kwanza kupata bao kupitia kwa Stuart Armstrong dakika ya 12 kisha Marcus Rashford akasawazisha dakika ya 20 na baadae Bruno Fernandes kumpa pasi ya mwisho Anthony Martial aliyefunga bao la pili dakika ya 23.
Wakati Mashabiki ya Man United wakitarajia mchezo kumalizika kwa matokeo hayo Michael Obafemi alisawazisha na kufanya mechi kumalizika 2-2 hivyo kuifanya Man United isalie nafasi ya tano ya msimamo kwa tofauti ya pointi moja na Chelsea mwenye pointi 60.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.