Home Makala Farid Mussa Atua Yanga

Farid Mussa Atua Yanga

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji aliyekuwa anakipga ndani ya CD Tennerife ya Hispania,Farid Mussa ametangazwa rasmi leo kuwa mali ya Yanga baada ya kumwaga wino wa kuitumikia klabu hiyo kwa dili la miaka miwili.

Mussa ameibukia ndani ya Yanga akiwa ni mchezaji huru baada ya dili lake la miaka minne ndani ya CD Tennerife kuisha na amekuja kuziba nafasi ya mnyarwanda,Sibomana ambaye alisitishiwa mkataba na yanga baada ya msimu wa 2019/2020 kumalizika.

Mkataba huo umesainiwa mbele ya mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM,Mhandisi Hersi Said ambao mbali na kuidhamini klabu hiyo pia imeamua kusimamia usajili ili kukiboresha kikosi cha yanga katika msimu ujao wa 2020/2021.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited