Home Makala Watatu Simba Kuikosa Ihefu Jumapili

Watatu Simba Kuikosa Ihefu Jumapili

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa Simba Sc,Sven Vandenbroeck amewachomoa nyota wake watatu ambao ni Luis Miqussone,Pascal Wawa na Chris Mugalo kwa kuwa hawakuwepo kwenye mazoezi ya awali na wachezaji wenzao kambini wiki mbili zilizopita.

Nyota hao watatu wanauwezekano mkubwa wa kuzikosa mechi mbili mfululizo baada ya kubakishwa Dar huku wanasoka wenzao wakiwa tayari wametua jijini Mbeya kujiandaa na mechi yao ya kwanza ya ligi kuu bara kwa msimu wa 2020/2021 dhidi ya Ihefu Jumapili,Septemba 6.

Kocha wa viungo,Adel Zrane amepewa jukumu kubwa la kuhakiksha wachezaji hao watatu wanakuwa fiti wakati wenzao wakiamsha popo katika mechi mbili za ugenini zitakazochezwa siku tofauti.

banner

Wengine waliobakishwa Dar ni kipa namba tatu Ally Salim na Crypin Kipenye ambaye alikuwa anasubilia dili lake la kwenda kwa mkopo Ihefu msimu huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited