Home Soka Yanga sc Yamrejesha Kocha wa Shikhalo

Yanga sc Yamrejesha Kocha wa Shikhalo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga imetangaza kumrejesha kikosini aliyewahi kuwa kocha wa makipa wa klabu hiyo Razak Siwa ambaye  raia wa Kenya ns anachukua nafasi iliyoavchwa na Vladimir Niyankuru aliyefutwa kazi hivi karibuni sambamba na aliyekuwa kocha mkuu Cedric Kaze.
Yanga pamoja na Siwa hawajaweka wazi mkataba ulioingiwa ni wa muda gani lakini kocha huyo amewahi kufanya kazi na Mlinda lango wa Yanga Farouk Shikalo wakati wakiwa katika timu ya Bandari Fc ya nchini Kenya ambako Farouk aling’ara kiasi cha kutwaa tuzo ya kipa bora wa msimu nchini humo.
Huu ni muendelezo wa klabu ya Yanga kuliimarisha benchi lake la ufundi ambapo kwa sasa timu imekabidhiwa kwa Juma Mwambusi Hadi mwishoni mwa msimu huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited