Home Soka Cas Yaibuka Kesi ya Morrison

Cas Yaibuka Kesi ya Morrison

by Sports Leo
0 comments

Mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kesi za michezo (Cas) wamesema kwamba kesi ya klabu ya Yanga sc dhidi ya mchezaji Benard Morrison itasikilizwa kuanzia tarehe 3 mwezi juni baada ya kujiridhisha kuwa kuna kesi ya kusuluhisha.

Cas wamewataka Yanga sc na Morrison kuwasilisha nyaraka za ushahidi ama kesi isikilizwe kwa kutumia nyaraka za awali ili kutoa hukumu ya kesi hiyo.

Kesi hiyo imechelewa kusikilizwa kiasi cha mashabiki wengi kudai ni ujanja wa viongozi wa Yanga sc kuficha udhaifu wao huku Yanga sc wakisema kesi imecheleweshwa baada ya mlalamikiwa Benard Morrison kudai kuwa kesi hiyo ilidishwe nchini ili isikilizwe na mamlaka za ndani ambapo shauri hilo limekataliwa na Cas.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited