Mabao mawili ya Feisal Salum dakika za 23 na 32 na lile la Saido Ntibanzokiza yalitosha kuipa Yanga sc alama tatu dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu nchini.
Matokeo ya mwisho ya mabao 3-2 yalionekana kutowafurahisha wanajangwani hao kiasi cha kusababisha mashabiki kumlaumu Metacha Mnata kutokana na kuruhusu bao la kizembe la pili lililowatia hofu mashabiki hao.
Mabadiliko ya kumtoa Mukoko Tonombe yalisababisha Yanga sc kukosa nguvu eneo la katikati huku kuingia kwa Emmanuel Martin kulisababisha Ruvu kuwa na madhara eneo la ushambuliaji.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.