Home Soka Yanga watangulia Kigoma

Yanga watangulia Kigoma

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Yanga imewasili tayari Kigoma kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa fainali wa kombe la shirikisho dhidi ya watani wao wa jadi klabu ya soka ya Simba.

Yanga imetua Kigoma asubuhi ya leo wakiwa na msafara watu 38 wakiwemo wachezaji 20,benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo na kupokelewa na msafara mkubwa wa mashabiki,wanachama na wapenzi wao wa mkoani huo wakiojitokeza kwa wingi kuilaki timu yao.

Yanga watacheza na Simba tarehe 25 Julai katika dimba la Lake Tanganyika katika mchezo wa fainali unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki na wadau wa soka nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited