Home Soka Makambo anukia Yanga sc

Makambo anukia Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Kidemokrasia ya Kongo Heritier Makambo anatajwa kukaribia kusajiliwa na mabingwa wa kihistoria wa Tanzania klabu ya soka ya Yanga.

Mchezaji huyo alitua nchini siku ya jana akipokelewa na baadhi ya mashabiki wachache wa klabu hiyo waliokuwepo kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere na kuzua hisia kwa mashabiki wa soka kuwa ametua kujiunga na timu hiyo ya zamani aliyoichezea kwa mafanikio makubwa kabla ya kutimkia Horoya ya Guinea.

Akiongea kwa njia ya simu na moja kati ya vituo vya redio Afisa habari wa Yanga Hassan Bumbuli amesema wananchi wajiandae muda wa wowote kabla ya siku kuisha kwani watatangaza usajili mpya,huku wadau wengi wakiamini ni wa Makambo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited