Home Soka TANZIA: MJUMBE KAMATI YA UTENDAJI YANGA AFARIKI

TANZIA: MJUMBE KAMATI YA UTENDAJI YANGA AFARIKI

by Sports Leo
0 comments


TIMU ya Yanga pamoja na familia ya wanamichezo duniani imepata pigo kufuatia kifo cha mjumbe wa kamati ya Yanga Felix Kibodya.
Kibodya amefariki usiku wa kuamkia leo Ijumaa hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela amethibitisha taarifa hizo za kifo cha Kibodya.
Mwakalebela amesema Yanga imepata pigo kutokana na msiba huo kwani walikuwa wanategemea nguvu kubwa kutoka kwa marehemu juu ya taaluma yake ya sheria.
Mwakalebela ameongeza kuwa kwa sasa klabu yao inafuatilia msiba huo kwa karibu kujua utaratibu kamili na kwamba baada ya hapo watatoa taarifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited