Home Soka Mwinuke ainukia Simba SC

Mwinuke ainukia Simba SC

by Sports Leo
0 comments

Winga wa klabu ya soka ya Gwambina Jimmyson Mwinuke amesajiliwa na mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC kwa mkataba wa miaka mitatu.

Mwinuke mwenye miaka 18 alikipiga Gwambina msimu uliopita na kuonyesha kiwango kizuri kilichowavutia wekundu wa Msimbazi ambao wanaamini atakuja kuwa mchezaji muhimu na mkubwa kwao.

Huu ni muendelezo  wa Simba SC kusajili vijana wadogo ambao wana umri mdogo ikiwa ni mpango wa kuja kuwauza hapo baadae mara baada ya kufanya biashara nzuri dirisha hili kwa kuwauza Chama na Miquissone.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited