Klabu ya Simbab sc imefanikiwa kupata sare ya mabao 1-1 dhidi ya klabu ya Olympique Club de Khouribga mchezo wa kirafiki wa kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu na michuano ya kimataifa uliofanyika katika kambi ya klabu hiyo nchini Morroco.
Kocha Didier Gomes aliwaanzisha Ally Salim,Gadiel Michael,Henock Inonga,Pascal Wawa,Pape Osmane Sakho,Sadio Kanoute,Benard Morrison huku pia Hassan Dilunga,Rally Bwallya na Chris Mugalu katika kikosi cha kwanza ambapo kilipata bao la kuongoza kupitia kwa Pape dakika ya 37.
Kipindi cha pili dakika za mwishoni Olympique Club de Khouribga walisawazisha na kufanya mchezo umalizike kwa suluhu huku makocha wa timu zote wakionekana kuwa bize na maandalizi ya vikosi vyao.
Huu ni mchezo wa pili wa kirafiki kwa klabu ya Simba sc ambapo mchezo wa awali walicheza na Far Rabat na kutoa sare ya mabao 2-2 huku kikosi hicho kikitarajiwa kurejea nchini wikiendi hii.