Home Soka Manara akaribishwa na wazee Yanga

Manara akaribishwa na wazee Yanga

by Sports Leo
0 comments

Msemaji mpya wa mabingwa wa kihistoria Tanzania Bara Haji Manara amekaribishwa rasmi makao makuu ya klabu hiyo Jangwani na wazee pamoja na viongozi mbalimbali timu hiyo katika tukio lilitokea hii leo.

Haji Manara baada ya kukaribishwa amesema kuwa ”ndugu zangu katika siku ngumu ni ambayo unapokewa na watu ambao unastahili kuwapokea,kwa mila na desturi zetu Afrika wazee wanapokewa na vijana,lakini kwa umaalumu mlionifanyia leo ni deni zito,sijawahi kupata mapokezi mazito kutoka kwa wazee wangu kama siku ya leo,deni hili pia ninalo kwa wanachama wote wa Yanga nchi nzima”.

Manara aliongeza ”nimerudi nyumbani sehemu ambayo imenikuza,mnafahamu wazazi wangu licha ya kucheza hapa lakini bado ni wanachama wa klabu hii na mimi kurudi hapa ni fahari kwamba narudi kufanya kazi katika klabu ambayo ilinilea na ndiyo klabu ya maisha yangu”.

banner

Msemaji huyo pia aligusia malengo ya klabu hiyo kuwa ni kutwaa mataji kwenye mashindani ya ndani pamoja na kufika hatua ya makundi katika michuano ya klabu bingwa Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited