Home Soka Hanspoppe aagwa Dar

Hanspoppe aagwa Dar

by Sports Leo
0 comments

Mwili wa aliyekua mjumbe wa bodi ya wakurugenzi ya klabu ya Simba na mjumbe wa kamati ya maadili ya TFF Zacharia Hans Poppe umeagwa mchana huu na wadau mbalimbali wa michezo hapa Tanzania katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.

Hanspoppe alifariki siku ya Jumamosi alipokua hospitali akipatiwa matibabu ya matatizo ya kupumua.

Zacharia atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwa klabu yake pendwa ya Simba kwa kuwa mmoja wa waandamizi walioiwezesha klabu hiyo kupata mafanikio makubwa ndani na nje ya nchi kwa miaka ya hivi karibuni,pia atakumbukwa katika mchango wake kwenye maendeleo ya mpira wa miguu hapa nchini.

banner

Baada ya kuagwa jijini Dar es salaam mwili wa mfanya biashara huyo maarufu utasafirishwa kwenda kwao Iringa kwaajili ya mazishi.

Mungu ailaze roho yake,mahali pema peponi,Amin

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited