Home Soka Stars yamaliza wa tatu kundi J

Stars yamaliza wa tatu kundi J

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imelazimisha sare ya 1-1 ugenini dhidi ya Madagascar mjini Atarsntananarivo na kumaliza wakiwa wa tatu katika msimamo wa kundi J kufuzu kombe la dunia Qatar 2022.

Stars ilianza kupata goli dakika ya 25 kupitia kwa mshambuliaji wa Wydad Casablanca Simon Msuva akimalizia pasi nzuri kutoka kwa kiungo wa Yanga Feisal Salum,kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 74 kupitia kwa mshambuliaji wao wa kati Hakim Abdallah akitumia vizuri makosa ya mabeki kushindwa kuundoa kwenye hatari mpira wa adhabu.

Katika mchezo huyo Tanzania ilimkosa nahodha wake Mbwana Samatta,beki wa kati Bakari Nondo na mlinda mlando Aishi Manula kutokana na kudaiwa kuwa na maambukizi ya UVIKO-19.

banner

Mchezo mwingine wa kundi hilo umeshuhudia DR Congo wakikata tiketi ya kumi 10 ambapo timu hizo zitamenyana kupata wawakilishi  5 kutoka Afrika kwenda michuano ya kombe la dunia itakayofanyika mwakani nchi Qatar.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited