Home Soka Cantona akosoa kombe la dunia

Cantona akosoa kombe la dunia

by Sports Leo
0 comments

Gwiji wa soka wa zamani wa Manchester united Eric Cantona ameoneshwa kukerwa na michuano ya kombe la dunia zitakazofanyika mwaka huu nchini Qatar  huku akiweka wazi kuwa hatajisumbua kuitazama.

Cantona ameyasem hayo alipokuwa kwenye mahojiano na gazeti la Independent la Uingereza.Alisema kuwa ”sielewi kwanini Qatar imechaguliwa kuandaa mashindano haya,Qatar siyo nchi ya soka,Marekani ni nzuri kwani kuna msukumo mkubwa kwa soka la wanawake hivyo lingefaa kwenda kwani lingesaidia zaidi ukuaji wa soka.

Hakuna ukuaji wa soka wa namna hiyo Qatar.Utaona ni kwa sababu za kifedha tu zimesababisha fainali zipelekwe huko,watu wengi wamekufa wakati wa uandaaji wa mashindao hayo.

banner

Aliendelea sijali,sitayaangalia kwakweli,siyo kombe la dunia kwangu binafsi,maisha ya watu yameharibiwa na bado sisi wengine tufurahie mashindano?haiwezekani”.

Kauli ya gwiji huyo huenda ikazua mijadala mbalimbali duniani hususani juu ya uhalali wa Qatar kupewa haki hiyo ya kuandaa ukizingatia ukandamizaji mkubwa wa haki za kibinadamu na sheria kali dhidi ya jinsia ya kike.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited