Home Makala Ibenge Hatarini Kutimuliwa

Ibenge Hatarini Kutimuliwa

by Dennis Msotwa
0 comments

Taarifa kutoka nchini Morocco zinasema kuwa endapo kocha wa RS Berkane, Florent Ibenge ambaye ni Raia wa Congo endapo atashindwa kuifunga Simba atafukuzwa kuwa kocha wa klabu hiyo katika  mchezo wa marudiano Jumapili kwenye uwanja wa Mkapa katika kombe la Shirikisho Afrika.

Ibenge alijiuga na Rs Berkane mwezi Julai mwaka jana akitokea klabu ya As Vita ya nchini Congo alipofundisha kwa miaka tisa anakabiriwa na kibarua kigumu kuwashawishi mabosi wa klabu hiyo kumbakiza klabuni hapo huku mechi hiyo dhidi ya Simba sc ikiwa ni mtego kwake ambapo akipoteza basi anaweza kutimuliwa.

Rs Berkane chini ya Ibenge imekua na mwendo wa kusuasua ambapo katika michezo 23 ya hivi karibuni imeshinda michezo nane pekee na kutoa sare michezo kumi huku ikifungwa katika michezo mitano.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited