Home Kikapu Nabi Yupo Sana Yanga sc

Nabi Yupo Sana Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Baada ya tetesi za muda mrefu kuwa anaweza kuondoka klabu hapo kocha wa Yanga sc Nasreddine Nabi amesaini mkataba mpya wa kusalia klabuni hapo kwa miaka miwili zaidi.

Nabi amesaini mkataba huo na kuzipiga chini ofa alizokuwa nazo kutoka klabu zenye hela za Far Rabat ya nchini Morroco na Al Hilal ya Sudan ambazo zilionyesha nia ya kumsajili.

Taarifa za ndani zinasema kwamba Nabi ameamua kubakia Yanga sc akiamini kuwa kutokana na uwekezaji uliofanywa kikosini humo anaweza kufanya makubwa katika ligi ya mabigwa barani Afrika ambayo klabu hiyo inashiriki msimu huu.

banner

Mbali na kukubali kusaini mkataba mpya pia maslahi ya kocha huyo yameongezeka kwa kiasi kikubwa huku ikisemekana atapokea zaidi ya milioni 30 za kitanzania kwa mwezi

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited