Home Makala 300m Zambakisha Beki Simba sc

300m Zambakisha Beki Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kiasi cha shilingi milioni mia tatu zilizotolewa na mabosi wa Simba sc zimefanikiwa kumbakisha beki Mohamed Hussein aliyekua na mpango wa kutimkia katika klabu ya Kaizer Chiefs ya nchini Afrika ya kusini.

Beki huyo tegemeo wa timu ya Taifa ya Tanzania alikua yupo mwishoni mwa mkataba wake klabuni hapo huku tayari akiwa na ofa nono ya Kaizer Chiefs waliokua wameweka kiasi cha milioni mia nne na mshahara wa milioni thelasini za kitanzania.

Mabosi wa Simba sc wakitumia nguvu kubwa ya ushawishi wamefanikiwa kuzima dili hilo na kumsainisha dili hilo jipya lenye thamani ya shilingi milioni mia kila mwaka kwa miaka mitatu huku wakimpatia mshahara wa shilingi milioni kumi kwa mwezi.

banner

“Haikuwa rahisi kwani, tayari Tshabalala alikuwa na ofa kubwa lakini viongozi wamekaa naye na kufanikiwa kumshawishi ili aweze kuendelea kuitumikia Simba kwa mafanikio kama alivyofanya tangu amejiunga na timu hii akitokea Kagera Sugar,”Alisema mtu wa ndani wa klabu hiyo ambaye hakutaka jina lake liwekwe hadharani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited