Klabu ya Simba sc ipo katika mipango mikali ya kusuka kikosi cha msimi ujao ambapo baada ya kumaliza msimu wakiwa katika nafasi ya pili ambapo Kipa Hussein Abel mbioni Kutemwa Simba Sc kutokana na uwezo wake kutoridhisha tangu amejiunga na klabu hiyo mwanzoni mwa msimu huu ulioisha.
Mabosi wa Simba wapo katika mchakato wa kutafuta kipa mwingine ambae atakuja kuziba nafasi ya kipa huyo msimu ujao na taarifa za awali zinaripoti kuwa wapo katika hatua nzuri za kunasa saini ya Kipa wa JKT Tanzania.
Abel alijiunga na Simba Sc akitokea klabu ya Tanzania prisons ya jijini Mbeya na wakati huu kuna vilabu kadha ambavyo vimeanza kuonyesha nia ya kuhitaji saini yake kwa ajili ya msimu ujao.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.