Home Makala Aubameyang Aipatia Arsenal Ubingwa

Aubameyang Aipatia Arsenal Ubingwa

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji Pierre Emerick Aubameyang ameifanya Arsenal kutwaa ubingwa wa kombe la FA mara ya 14 baada ya kuwafunga Chelsea mabao 2-1 kwenye mchezo wa fainali ya kombe la FA kwenye uwanja wa Wembley.

Chelsea walianza kupata bao la kwanza dakika ya tano kupitia Christian Pulisic ambaye alishindwa kumaliza dakika 90 za mchezo kutokana na kupata majeraha.

Arsenal walisawazisha bao hilo kupitia Aubameyang dakika ya 23 kwa mkwaju wa penalti huku bao la pili kutoka kwa raia huyo wa Gabon lilifungwa dakika ya 67.

banner

Chelsea walimaliza mchezo wakiwa pungufu kwani Mateo Kovacc alionyeshwa kadi za njano mbili na mwamuzi Anthony Taylor akifuatiwa na nyekundu baada ya kucheza rafu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited