Home Makala Azam Fc Yaweka Rekodi Ligi Kuu

Azam Fc Yaweka Rekodi Ligi Kuu

by Dennis Msotwa
0 comments

Azam Fc imezidi kujiwekea rekodi nzuri ndani ya msimu huu mpya wa ligi kuu bara 2020/2021 baada kufika raundi ya sita pasipo kufungwa wala kutoa sare ya kufungana.

Kikosi hicho kinachoongozwa chini ya kocha mkuu, Arstica Ciaoba kimefikisha jumla ya pointi 18 baada ya kunyakua pointi 3 hapo jana Octoba 15, kwa kuwatungua Mwadui Fc 3-0 uwanja wa Azam Complex.

Mabao mawili ya Azam Fc yalipachikwa na Obrey Chirwa dakika ya 28 na 63 huku yule kinara wao wa mabao Prince dube alitupia bao dakika ya 61.

banner

Azam Fc kwa sasa inashika usukani ikiwaacha mabingwa watetezi wa ligi kuu bara,Simba Sc nafasi ya pili wakiwa na pointi 13 kibindoni katika michezo mitano waliocheza nakufunga mabao 14 pekee kupitia safu yao ya ushambuliaji.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited