Home Makala Banda Apewa “Thank You” Simba sc

Banda Apewa “Thank You” Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Winga Peter Banda ametemwa rasmi na klabu ya Simba sc ikiwa ni baada ya misimu miwili tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea  katika klabu ya Nyassa Big Bullet ya nchini kwao Malawi ambako pia alikua kwa mkopo akitokea klabu ya FC Sheriff Tiraspol ya nchini Moldovia.

Banda alitegemewa kuwa mmoja wa mastaa watakaofanya vizuri klabuni hapo lakini hata hivyo ameshindwa kufanya mambo makubwa tofauti na matarajio hasa akisumbuliwa zaidi na majeraha ya mara kwa mara kiasi cha kocha Robertinho kuamua kuachana nae.

Simba sc imeachana na Banda huku nafasi yake ikizibwa na Jose Luis Miqquisone ambapo pia msimu huu imefanikiwa kuwanasa baadhi ya mawinga kama Leandre Onana na Aubin Kramo ambao wanatarajiwa kufanya makubwa zaidi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited