Mshambuliaji wa zamani wa Kagera Sugar,Kassim Khamis aliyechomoa dili la kujiunga na vigogo wa Kariakoo Simba na Yanga anapata tabu sana ndani ya Azam FC baada ya kuwekwa benchi kwa mrefu.
Licha ya makocha wawili kumkuta Kassim  aliyeanza na Etienne Ndayiragije ambaye kwa sasa yupo na timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kisha Arstica Cioaba ila hana nafasi kikosi cha kwanza.
Kassim amesema kuwa haelewi sababu ya yeye kukaa benchi na hawezi kuzungumzia suala hilo kwani lipo chini ya uongozi wake japo ni kwa muda hana nafasi kwenye kikosi cha kwanza kama awali.