Home Makala Bilionea Aitema Chelsea

Bilionea Aitema Chelsea

by Sports Leo
0 comments

Mmiliki wa klabu ya Chelsea fc Billionaire wa Urusi Roman Abramovich  ameikabidhi klabu ya Chelsea mikononi mwa bodi ya wadhamini wa klabu hiyo yenye maskani yake jijini  London nchini Uingereza.
 Hii inakuja siku moja baada ya wabunge wa bunge la Wingereza  kumtaka tajiri huyo kuachana na klabu hiyo kutokana na ukaribu wake na Rais wa Russia Vladimir Putina ambaye anapingwa na mataifa ya magharibi kutokana na kuamua kuivamia kijeshi nchini ya Ukraine kutokana na tofauti za kiitikadi baina ya nchi hizo mbili.
“Kuanzia leo ninawapa bodi ya wadhamini wa Chelsea usimamizi na utunzaji wa klabu nikiwa na imani wataisimamia vizuri huku nikiwakabidhi kila kitu kuanzia wachezaji,wafanyakazi na miundo mbinu yote”Alisema tajiri mwenye uraia wa Urusi Roman Abramovic

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited