Home Makala Caf Yaipa Mzuka Simba sc

Caf Yaipa Mzuka Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Simba wamepata mzuka wa aina yake baada ya CAF kuruhusu kuingiza mashabiki zaidi ya nusu kwenye Uwanja wa Mkapa Jumapili dhidi ya Berkane katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika.

Habari za ndani kutoka Simba sc zinadai kwamba uongozi wa klabu hiyo waliomba Shikirikisho la Soka Afrika (Caf) waingize mashabiki 60,000 ili kujaza uwanja katika mchezo wa wikiendi dhidi ya Berkane ya Morocco.

Hata hivyo, Caf imewapa mashabiki 35,000 ambao ni zaidi ya nusu ya uwanja huo unaobeba mashabiki 60,000 hivyo kuwapa ahueni kutokana na umuhimu wa mashabiki viwanjani huku Simba sc ikihitaji kushinda ili kujiwekea mazingira sawa ya kufuzu kutokana na kupoteza mchezo wa awali kwa Berkane kwa kipigo cha mabao 2-0.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited