Home Makala Dili La Kagere Hispania Limefikia Hapa

Dili La Kagere Hispania Limefikia Hapa

by Sports Leo
0 comments

Patrick Gakumba ambaye ni wakala wa nyota wa Simba Sc, Meddie Kagrer amefunguka kwamba dili la mchezaji wake kutakiwa na klabu ya Hispania limekuwepo na kitu pekee ambacho kinakwamisha suala hilo ni mabosi wa  Simba.

Wakala huyo alipata dili hilo baada ya kuzungumza na rafiki yake ambaye anaishi Hispania ambapo alikuwa anataka ampeleke straika huyo kwa ajili ya mkopo ambao angeweza kununuliwa moja kwa moja.

“Rafiki yangu anayekaa Hispania ndiye ambaye aliniambia kuwa moja ya klabu za ligi kuu ya nchi hiyo inamtaka Kagere kwa ajili ya mkopo na kama akifanya vizuri basi angeweza kusajiliwa moja kwa moja hivyo kwa sasa wanasubiri majibu kutoka uongozi wa Simba ambao wanashikilia mkataba wake”alisema Patrick

 

banner

Licha ya jina la klabu hiyo kufichwa, inaelezwa kuwa ni Levante ndiyo inayomhitaji straika huyo na endapo dili hilo litashindikana litafanya kagere kukosa  fedha nyingi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited