Home Makala Dtb Wamvizia Wawa

Dtb Wamvizia Wawa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Dtb iliyopanda kucheza ligi kuu msimu ujao inaangalia uwezekano wa kumsajii beki wa klabu ya Simba sc Serge Paschal Wawa endapo klabu hiyo itaaamua kutomuongezea mkataba mpya baada ya mkataba wa sasa kuelekea ukingoni.

Klabu hiyo inayodhaminiwa na benki ya Dtb inaamini kuwa uzoefu wa beki huyo ni kitu muhimu sana kwa maendeleo ya klabu hiyo kunako michuano ya ligi kuu nchini huku akiwa na uzoefu wa kukutana na washambuliaji hatari wa ligi kuu na wale wa kimataifa.

Wawa anamaliza mkataba wake na klabu ya Simba sc ambayo mpaka sasa haijaonyesha nia ya kumsainisha mkataba mpya baada ya kutua klabuni hapo misimu mitatu nyuma akitokea nchini Sudan.

banner

Uwepo wa Joash Onyango na Henock Inonga ndio sababu kuu ya Wawa kukosa nafasi kikosini humu ambapo mara nyingi hukaa benchi ama kucheza michezo michache endapo mmoja katika mabeki hao anapokosekana.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited