Home Makala Dtb Yabadili Jina

Dtb Yabadili Jina

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya DTB iliyopanda kucheza ligi kuu nchini imebadili jina na sasa itajulikana kama Singida Big Stars huku ikihamisha makao makuu yake kutoka jijinin Dar es salaam kwenda mkoani Singida.

Timu hiyo imepanda kucheza ligi kuu msimu ujao ikiwa sambamba na Ihefu Fc baada ya kushika nafasi ya pili ambapo baada ya uamuzi wa kubadili jina hilo sasa itaitwa Singida Big Stars na itatumia uwanja wa Liti kama uwanja wake wa nyumbani.

Uamuzi wa klabu hiyo kubadili jina na kuhamia mkoani Singida umetangazwa leo na uongozi wa klabu hiyo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited