Home Makala Eymael Akamuliwa Milioni 8 Tff

Eymael Akamuliwa Milioni 8 Tff

by Sports Leo
0 comments

Kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka Tanzania (TFF) imemfungia miaka miwili aliyekuwa kocha mkuu wa Yanga Sc , Luc Eymael kujihusiana na masuala ya soka Tanzania pia kutozwa faini ya Shilingi milioni 8.

Eymael amekutana na pigo hili kutokana na makosa ya ubaguzi pamoja na uchochezi ambao aliufanya baada  ya mchezo wa mwisho wa ligi kuu bara dhidi ya Lipuli uliochezwa Julai 26 Uwanja wa Samora mkoani  Iringa.

Kosa hilo lilimpelekea kocha huyo Mbelgiji kufufutwa rasmi kazi na Yanga, Julai 27 na kwa sasa yupo zake Ubelgiji.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited