Home Makala Farid Ajifunga Miwili Yanga sc

Farid Ajifunga Miwili Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo Farid Musa Malick amesaini  mkataba wa miaka miwili kuendelea kusalia katika klabu ya Yanga sc mpaka mwaka 2024baada ya ule wa awali kuelekea ukingoni mwishoni mwa msimu huu.

Farid ametambulishwa leo mbele ya waandishi wa habari kuwa amesaini mkataba huo akiwa chini ya meneja wake mpya Oscar Oscar na kuzima maswali ya wadau wa soka ambao walikua wakijiuliza kama bado ana ndoto za kusaka timu nje ya nchi.

Awali wakati anajiunga na klabu hiyo miaka miwili iliyopita staa huyo alinukuliwa akisema kwamba ana mpango wa kwenda nje ya nchi kucheza soka lakini atasalia nchini kwa muda kutokana na Janga la Corona lililosababisha akose timu ulaya na hivyo akaamua kujiunga na Yanga sc.

banner

Hata hivyo Farid ndani ya kikosi cha Yanga sc amefanikiwa kumvutia kocha Nasredine Nabi ambaye amekua akimtumia kama kiraka katika nafasi za beki wa pembeni,kiungo na winga hivyo kuongezewa mkataba wa kusalia jangwani lilikua ni jambo lililotarajiwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited