Home Soka Farid,Yao Kuwakosa Kagera Sugar

Farid,Yao Kuwakosa Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wawili wa klabu ya Yanga sc Farid Mussa na Yao Kouasi Attouhoula wanatarajiwa kuukosa mchezo wa Ufunguzi wa ligi kuu kwa klabu yao dhidi ya Kagera Sugar Fc utakaofanyika August 29 katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera.

Kikosi cha Yanga sc tayari kimewasili mkoani humo huku mastaa hao wakiachwa jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na majeraha ambapo Yao mpaka sasa anaendelea vizuri na yupo karibuni kurejea kikosini.

Kwa upande wa Farid Mussa yeye anatarajiwa kufanyiwa upasuaji ili kupona jeraha lake ambapo anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili.

banner

Kikosi cha Yanga sc baada ya kumaliza michuano ya kimataifa ya klabu bingwa barani Afrika hatua ya awali sasa kimerejea kwa ajili ya ligi kuu nchini na kitavaana na Kagera Sugar katika mchezo huo wa kwanza wa ligi msimu huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited