GSM imejiondoa Rasmi kuwa mdhamini mwenza wa Ligi Kuu Tanzania bara kutokana na kutotimizwa Kwa Makubaliano ya Mkataba baina yao na Shirikisho la soka nchini (TFF).
Kampuni hiyo ambao ni wadhamini wenza wa Ligi Kuu Bara wametangaza kujitoa kudhamini ligi hiyo leo Februari 7 ikiwa ni siku 76 tangu wasaini mkataba wa Sh2.1 bilioni Novemba 23.
Gsm katika mkutano wake na waandishi wa habari nchini wametangaza kujitoa kutokana na bodi ya ligi kuu nchini (TPLB) pamoja na Tff kushindwa kukamilisha masharti ya kimkataba ambao waliingia na kampunin hiyo ikiwemo klabun zote kuvaa nembo ya kampuni hiyo mabegani.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mkuu wa GSM Ghalib Mohamed amejiuzuru kuwa Mwenyekiti wa kamati ya Ushindi ya Taifa Stars.