Home Makala Hapatoshi Namungo Ikiwasili Kagera

Hapatoshi Namungo Ikiwasili Kagera

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Namungo Fc maarufu kama Wauaji wa Kusini  tayari wamewasili mjini Bukoba kwa ajili ya mchezo dhidi ya Kagera sugar utakaopigwa uwanja wa kaitaba siku ya Jumatano Oktoba 4,2023.

Namungo wamewasili mkoani humo kwa ndege wakiwa na mastaa wote hasa wale waliocheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga sc walipofungwa 1-0 licha ya kufanikiwa kucheza vizuri mchezo huo na kutoa ushindani wa kutosha kwa mabingwa watetezi wa ligi kuu nchini.

Namungo Fc wanapaswa kushinda mchezo huo ili kujikwamua kutoka mkiani ambapo mpaka sasa wana alama mbili pekee baada ya kupata sare mbili na kufungwa michezo miwili kati ya minne ya ligi kuu mpaka sasa huku Kagera Sugar wakiwa na alama nne katika michezo minne ya ligi kuu.

banner

Katika michezo ya mwisho Kagera Sugar walipata sare dhidi ya Jkt Tanzania huku Namungo Fc wakipata suluhu nyumbani dhidi ya Mashujaa Fc ya Kigoma.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited