Abdulhalim Humud wa Mtibwa Sugar amejiunga na Namungo Fc leo Agosti 13 iliyo chini ya Hitimana Thiery kwa dili la miaka miwili.
Humud akiwa Mtibwa Sugar msimu wa 2019/20 alihusika kwenye jumla ya mabao mawili kati ya 30 ambapo alifunga mabao mawili ndani ya kikosi hicho.
Namungo FC itashiriki michuano ya Kimataifa baada ya kutinga hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho na kucheza na Mabingwa wa Ligi Kuu Bara ambao ni Simba hivyo itaiwakilisha nchi kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.